Tulikua tunakaa na wazazi wangu Tabora na nilimaliza shule ya sekondari kule alafu nikaja kusoma mpaka chuo Dar es salama. Nilikua nasomea mambo ya biashara huko chuo na nilienda chuo baada tu ya kumaliza sekondari. Nilipokua chuo nilikua na rafiki yangu mmoja anaitwa Jimmy. Huyu jamaa tulikua marafiki sana kwasababu tulikua tumetokea sehemu moja. Na yeye alikua ametokea Tabora. Alikua ni muongo jamaa huyu ingawa mimi nilimzoea lakini alikua muongo sana. Pamoja na kwamba nilikua rafiki yake lakini alikua hawezi kuniambia vitu vya ukweli. Ilikua ni kawaida kwake kukwambia “Nisubiri nakuja” na hasije, “Niazime hela nitakurudishia” na asirudishe au “Nipo Sehemu flani” na asiwepo hiyo sehemu. Lakini alikua bado ni rafiki yangu na tulikua tunakaa chumba kimoja kilichokua pembezoni kidogo ya chuo. Uongo wa Jimmy ulikua kunamda unaniudhi mimi na hata watu wengine lakini kwake ulikua na faida. Alikua na anakamata sana madada wa pale chuoni. Alikua anapendeza kwa nguo za kuazima azima kwa watu na watu wengi hapo chuoni walikua wanahisi anatoka sehemu yenye hela sana lakini kiukweli alikua ananitegea sana kwenye swala la pesa maana kwao walikua hamampi hela sana kama ninavyopewa mimi. Kwakua alikua ni rafiki ilikua sio shida.
Wakati naanza chuo nilijikuta navutiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na dada mmoja mzuri na alikua anafahamika sana kwa uzuri hapo chuo. Moyo wangu ulimpenda huyo dada na sikuwahi mwambia hata rafiki yangu Jimmy kuhusu huyo dada. Alikua anaitwa Zuwena na watu wanamuita “Zuu” badala ya kulitaja jina lake lote. Alikua ni dada flani hivi mweusi alafu anaumbo zuri sana. Alikua amebalikiwa sura nzuri na nyuma alikua amejaza sana kiasikwamba alikua akitembea unajikuta unavutiwa kumuangalia jinsi mizigo inavyojitikisa.
Nilitamani sana kumwambia hisia nilizo nazo juu yake lakini tulikua hatuna ukaribu nae kabisa na pia nilikua na uwoga. Zuu alikuana marafiki wengi warembo kama yeye wanaomzunguka mara kwa mara na mmoja ya marafiki zake alikua anaukaribu kidogo na mimi. Huyo rafiki yake alikua anaitwa Sara na alikua ni mpole kidogo kuliko marafiki wengine wa Zuu. Ukaribu wangu na Sara ulikua wakusalimiana na kuongea maneno mawili au matatu tu kutokana na kwamba tuliwahi kaa karibu kwenye mthihani wa kujipima akaniomba nimsaidie kidogo, nikamsaidia.
Basi mimi bila kuwaza mbali nikaona bora niongeze ukaribu na Sara ili nipate nafasi ya kuwa karibu na Zuu na kwakua zuu ni rafiki wa Sara basi nikaona huenda nitakua najua mambo mengi ya Zuu kupitia kwa Sara. Niliongeza ukaribu na Sara kasikwamba tulikua tunawasiliana kila siku na ananitafuta kila muda tukiwa chouni, kwenye simu au nje ya chuo. Ukaribu huo ulileta matokeo ambayo sikuyatarajia maana ilifikia kipindi nataka kumuuliza Sara mambo ya Zuu lakini kila nikijaribu kuingizia mada za Zuu au mwanamke mwengine, anazutupilia mbali alafu anakua kama anachukia hivi. Hali hiyo iliendelea mpaka kunasiku moja hivi nilikua nimekaa chuoni nimejitenga najisomea nikakuta Sara amekuja kukaa na mimi. Ni kawaida yake kufanya hivyo. Tulipiga stori hapo za uongo na ukweli ila katikati ya stori nikashangaa kumuona Sara kaganda tu ananiangalia usoni kwa macho ya kulegea bila kuongea kitu. Mimi kuona hivyo nikasema kwa kisauti cha chini “We Sara… Ndo nini hivyo?… wewe unaniangaliaje hivyo?… wewe” nikakuta bila kuyayumbisha macho yake anasema “Niangalie vizuri machoni’. Nilivyosikia hivyo nikaacha kumuangalia macho, nikaangalia kulia na kushoto kwanza kama kunamtu anatuangalia muda huo maana macho ya Sara yanaonesha ni mtu aliechoka kuzificha hisia zake juu yangu na yupo hapo kunionesha jinsi anavyo hisi. Niliona amna mtu anaetuangalia muda huo, nikayarudisha macho kwa Sara nikasema “Macho yako mbona kama… Mbona kama yako vizuri tu ila yanakua kama unausingizi hivi”. Akaniambia “Endelea kuniangalia tena alafu niambie umegudua nini”. Mimi nikimuuliza “Macho yanakuuma?” akakataa kwa kutikisa kichwa. Nikatulia kidogo nikamuuliza “Unanipenda?” nikakuta anakubali kwa kutikisa kichwa chake huku akiwa na vimacho kama anataka kudondosha vimachozi hivi. Nikamwambia “Ah sasa kumbe ndio hicho kinakufanya uniangalie hivyo… Na mimi nakupenda… nipe mkono wako nikwambie kitu”. Basi nikaona Sura yake inatabasamu kubwa sana baada ya mimi kusema hivyo. Tulishikana mikono tukaanza kuongea vitu vya upendo upendo pale tukiwa na kauwoga uwoga maana sehemu hiyo ilikua sio sehemu sahihi kwa watu kushikana shikana. Tulitaka kukutanisha midomo lakini sehemu hiyo haikua inaruhusu sisi kufanya jambo hilo. Kwanzia siku hiyio mimi na Sara tulikua wapenzi ila kiukweli mimi moyoni mwangu bado nilikua nampenda Zuu na sio Sara. Pamoja na kwamba nilikua kwenye mahusiano na Sara na ananipa raha kila nikizihitaji lakini bado nilikua naiwinda nafasi ya kuwa na Zuu.
Kunasiku nilipata nafasi ya kuongea na Zuu kidogo akiwa pekeyake na nikaitumia kumuomba namba ya simu tu. Siku hiyo hiyo nikamcheki kwenye simu mida ya jioni. Nilijitambulisha kuwa ndie niliemuomba namba akasema amenikumbuka ila hatukuongea sana akasema “Subiri kidogo nitakushtua, kunakitu nafanya”. Nilisubiri sana nikaona mpaka naingia kulala hajanitafuta. Sana sana nilikua nikisumbuliwa na Sara tu kwenye simu akidai nimebadilika nimekua kama simpendi hivi. Nilimpuuza Sara nikaona nijaribu kumtumia ujumbe Zuu ili kama amesahau akumbuke lakini nikakuta hajibu mpaka asubui inafika.

Siku iliofuata nikaenda chuo na nikatafuta sana nafasi ya kuongeanae na bahati nzuri niliipata tena. Nakumbuka nilimuona amekaa pekeake sehemu anaandika. Nilivyomuona nikaangalia kulia na kushoto kuhakikisha Sara hayupo maeneo yale alafu nikamfuata. Alikua amependeza alafu nguo ya juu aliokua ameiva ilikua imeacha kinafasi kinachoonesha tunda za kifua chake zikiwa zimebanana kiasikwamba nilikua kila nikizitupia macho mapigo yangu ya moyo yalikua yanaongezeka. Nipofika nikasema “Mambo vipi Zuu” akaacha kuandika akaniangalia akanijibu “Safi tu, Mzima?” mimi nikamwambia “Nimekuona toka kule upo bize sana kuandika, unaandika nini?” akasema “Mh kunavitu nahamisha toka kwenye daftari hili hapa” nikasema “Anha sawa, nimekuja kukusaidia kuandika”. Kusikia hivyo akasema “Hahaha, namaliza mwenyewe hizi usihofu banaa… Nimeanza kuandika tangu jana, leo namalizia tu” mimi nikasema “Haya” alafu nikasema tena “Alafu jana nimekutafuta ukasema utanitafuta lakini hukunitafuta” nikakuta ananijibu “ah hahaha hivi nilikwambia nitakutafuta? dah nilisahau kabisa alafu jana tulivyoongea tu, nikaweka simu kwenye chaji… nimekuja kugusa leo wakati nakuja huku na nimekuta SMS nyingi bado sijasoma ila tutaongea vizuri leo, nitakutafuta”. Alivyoniambia hivyo nikamwambia “Sawa” tukapiga stori kidogo sana alafu nikamuacha pale aendelee kuandika.
Kiukweli Zuu japokua ilikua tukikutana tunaongea lakini niligundua ni mtu anaenidharau sana na ananikwepa maana hata siku hiyo bado hakunitafuta na hata nilipomtafuta, nikawa sijibiwi chochote. Jambo hili lilinifanya mpaka niwaze “Huenda Zuu anajua ninachotaka kwake na anajua ninamahusiano na rafiki yake Sara au tu anaona simuwezi… kwanza kwa muonekano wake tu anaonekana anataka watu wakubwa wenye pesa za kutosha”. Nilivyoona ananisumbua sana akili yangu nikaona isiwe taabu, acha nitulie na Sara tu maana kipindi hicho Zuu alifanya nimpuuze sana Sara. Niliacha kumfuatilia Zuu, nikajikita zaidi kwa Sara lakini nilikua bado natamani niwe na Zuu kimapenzi kama ningepata nafasi.
Baada ya kama wiki moja hivi toka niache kumfuatilia Zuu nilikutana na kitu ambacho sikukitegemea kabisa. Ilikua ni jumamosi mida ya saa 9 mchana nilikua nipo kwenye chumba tunachokaa na rafiki yangu Jimmy. Muda huo Jimmy alikua hayupo, aliondoka toka asubui akiwa amependeza sana na hakuniambia anakoenda na wala sikumuuliza maana hata nikimuuliza huwa haongei ukweli. Kuliko kukaa tu humo nikaona bora nikusanye nguo zangu chafu zilizokua zimezagaa chini zimejichanganya na za jimmy nifue. Wakati nakusanya nguo ghafla mlango ukagongwa “Ngo ngo ngo” na sauti ya Jimmy akisema “Oi wewe”. Niligundua ni Jimmy nikasema “Oya… Umerudi sasa haha” akawa anasukuma malango huku anasema “Ahaha nimekuja na shemeji yako huyu” huku akimruhusu mtu aingie. Mimi nikatupa macho kuangalia mtu anaeingia ni nani, nikakuta ni Zuwena amevaa nguo nyeusi fupi alafu inaangaza kiasi ambacho baadhi ya sehemu zake za mwili zinaonekana na Jimmy alikua anamshika kiuno alipokua akiingia ndani. Nilipomuona Moyo wangu ulidunda kwa mshtuko “Nduh” na nikahisi kama kuishiwa nguvu hivi…
INAENDELEA…
Hii ni simulizi ya UTAMU WA JUMLA ilio katika maandishi. Ina uhusiano kidogo na Simulizi ya SUKARI YA DADA na MZIGO WA WAKUBWA. Inapatikana katika Sauti pia. Inavipande 11.
Tutumie ujumbe WhatsApp upate simulizi zote
6 thoughts on “UTAMU WA JUMLA 01 (Simulizi ya maandishi)”