Matumizi ya internet katika ulimwengu wa sasa yamekua ni makubwa sana. Hadi kufikia mwaka 2024 mwezi Julai, Asilimia 67.1 ya watu Duniani walikua wanatumia internet. Asilimia hiyo ya watumia internet ni sawa na kusema watu billioni 5.45 wanatumia internet hapa Duniani. Hii yote ni Sababu internet imekua ikirahisisha mambo mengi katika maisha ya binadamu na kuwa muhimu kwenye mambo mengine mengi anayofanya kwenye Duniani ya sasa.
Katika kutumia internet, watu wanao ongoza kutumia internet ni wamiliki wa simu za mkononi. Simu za mikononi zimekua ni kati ya vifaa ambavyo watu huvutumia zaidi katika matumizi ya internet kuzidi PC. Asilimia kuwa ya watu hawa hutumia internet kupata habari na kujiunga na ndugu au marafiki kupita mitandao ya kijamii.
Katika mitandao ya kijamii ukiwa sehemu yoyote, yawezekana ukawa kutana na watu wakiongelea vifurushi vya internet vya bei rahisi. Baadhi ya wanao zungumiza vifurushi, huongelea vifurushi vya SME. Hapa tunaenda kuvizungumzia vifurushi hivi ili kuwapa mwanga watu wasio vijua.
Vifurushi vya SME
Kabla ya kufahamu moja kwa moja vifurushi hivi, unapaswa kufahamu maana ya SME. SME ni kifupi cha maneno ya Lugha ya kiingereza ambayo ni “Small and Medium-sized Enterprises” yenye maana “Biashara Ndogo na za Kati”. Kwamaana hiyo, “Vifurushi vya SME” ni vifurushi kwaajili ya Biashara Ndogo na za Kati.
Faida ya vifurushi vya SME
Mitandao ya simu kama Vodacom, Tigo, Halotel na Airtel imekaua ikitoa vifurushi vya internet, dakika na SMS kwaajili ya Biashara Ndogo na za Kati(SME). Vifurushi hivyo hupatika kwa bei rahisi ukilinganisha na vifurushi vya kawaida.
Vifurushi hivi vimekua ni msaada mkubwa kwa wafanya bishara kwa kupunguza gharama wanazotakiwa kutumia kupata SMS, Dakika na internet katika shughuri zao za kibiashara.
Katika upande wa internet, vifurushi vya biashara vinaweza kumsaidia mtu kupata vifurushi vikubwa vya internet kwa bei ndogo. Hii ni moja ya sababu watu wengi huviongelea katika mitandao ya kijamii.
Upatikanaji
Ukihitaji kupata vifurushi vya biashara kwenye mtandao wa Simu unaoutumia (Vodacom, Airtel, Halotel au Tigo, unaweza anza kwa kuwasiliana na kampuni inayokupa huduma. Tuma maelezo kwenye kurasa zao za kijamii au wapigie na uwaulize kuhusu utaratibu wa kupata huduma ya vifurushi vya biashara.
Kama itawezekana, unaweza tembelea katika maduka yao maalumu ili kufuata utaratibu wa kupata vifurushi hivi.
Mara nyingi huwa wanahitaji uthibitisho wa taalifa zako na vitu kama TIN number. Uhitaji wa vitu hivyo, huwa unatofautiana kidogo.
Baadhi ya watu ambao hawana muda wa kufuatilia mpaka kuvipata vifurushi hivi, huwatumia watu wa mitandaoni ili kujiunga na huduma hii. Kutumia watu kupata vifurushi vya SME ni wazo zuri japo ni hatari sana kutokana na uwepo wa matapeli mtandaoni.

Ukihitaji mtu wa uhakika kukuunga katika Vifurushi vya SME ili kupata internet, dakika na SMS kwa bei rahisi, unaweza tumia ujumbe kwenye WhatsApp tukakusaidi kupata huduma hii kwenye baadhi ya mitandao.