Sababu 5 za kukataliwa na Wanawake

Kukataliwa na wanawake ni jambo linaloweza kumkuta mwanaume yeyote, na mara nyingi linaweza leta huzuni na kuchanganyikiwa kabisa. Katika mambo mwanaume huogopa katika Maisha yake, kukataliwa na mwanamke ni moja wapo. Mwanaume anaweza mzawadia zawadi ya thamani mwanamke bila kumwambia anampenda kwasababu ya woga wa kukataliwa tu.


Kipindi cha nyuma baadhi ya wanaume wasio amini kuwa kuna maisha ya furaha baada ya kukataliwa na mwanamke, walikua wanajitupa hata kwenye maamuzi mabaya baada ya kukataliwa. Lakini kwa sasa watu wengi wameelimika na wanaamini kuna maisha yanaendelea baada ya kukataliwa na mwanamke.


Sababu za mwanaume kukataliwa ni nyingi na huwa tofauti. Na sio kila mwanamke husema Sababu ya kumkataa mtu, wengine huficha.
Katika Sababu hizo tofauti, kuna mambo au sababu huwa zinajirudia na wanaume wengi hukataliwa kwasababu hizo. Kama ni mtu ambae upo katika kipindi cha kutafuta mwenza wako, itakua vizuri kuzihafamu sababu hizi.


Kuzifahamu au kuzijua hizi sababu kunaweza kusaidia kuboresha mbinu zako za kumpata mwanamke unaempenda maishani. Katika makala hii ya The bestgalaxy, tunaenda zungumzia baadhi ya sababu zinaweza kusababisha mwanaume kukataliwa.

Sababu 5 za kukataliwa na Wanawake

Usafi au kutojipenda

Inasemekana kuna wanawake wengi wanavutiwa na mwanaume msafi anaejipenda. Kati yao, wanawake wengine huwa wanafikili mwanaume msafi ana anaejipenda anaweza kuwajali kama anavyojijali. Hapa ndio mara nyingi wanaume wanaoitwa “Mabishoo” huwa juu.


Usipo kuwa msafi na unaejipenda, unaweza kukumbana na changamoto za kukataliwa sana na wanawake. Mwanamke anaweza asikwambie moja kwa moja, lakini tatizo au sababu ya kukataa ikawa ni hiyo.

Kumuhitaji sana


Mwanamke anaweza sema anamtaka mwanaume anaempenda na kumjali lakini akawa na Wanaume wengi wanaomkata na wanapambana kumpata kwa kumfanyia vitu vingi vya kumjali ili awakubalie lakini anawakataa. Cha kushangaza, mwanaume ambae anaweza uteka moyo wa mwanamke wa namna hii anaweza kuwa ni mwanaume asieonesha kumuhitaji sana kama wengine.


Kiufupi baadhi ya wanawake hawataki mwanaume aoneshe uhitaji sana. Wanataka mwanaume anaewapa muda, anaewapa vimashaka mashaka kidogo lakini anaupendo wa kweli.
Kuonesha kumuhitaji sana mwanamke, kunaweza kufanya uonekane mjinga kwake na ukakataliwa.

Kutokujiamini

Wanawake wengi huvutiwa na mwanaume anaejiamni. Kujiamini kwenye maisha na mambo yako ukiwa kama mwanaume, kunaweza fanya wanawake wengi kuvutiwa na wewe alafu wakakukabari.
Usiwe ni mtu unaeonesha kutokujiami mbele ya wanawake. Kuna wanawake huchukizwa sana na mwanaume ambae hajiamni hata kwakuongea kinyonge tu kunaweza mchukiza.


Ukiwa ni mwanaume unaejiamni, mwanamke anaweza kukukubali na kuamini katika wewe. Kiufupi ukijiamni, wanawake watakuamni. Lakini katika kujiamni kwako hakikisha unaepuka kujisifu sana kwake.

Muelekeo wa maisha

Mwanaume anaweza mtongoza mwanamke bila kufikilia mbali kuhusu mahusiano na maisha. Lakini mwanamke anaweza mkubali mwanaume baada ya kufikilia mbali sana kuhusu maisha na mahusiano.


Mwanaume mwenye maisha mazuri au anaeweza kupambana kupata maisha mazuri anakua na nafasi kubwa ya kukubaliwa na wanawake. Unaweza mwanaume usiwe na pesa nyingi lakini upambanaji wako wa Maisha na muelekeo wako ukawa ni mzuri kiasi, utakubaliwa kirahisi.

Kukata Tamaa ya jibu zuri


Kuna wanaume hukata tamaa ya kuendelea kumfuata mwanamke ambae amekataa kuwa nae mara moja tu. Ukiwa ukiwa Mwanaume unaekata tamaa kwa kukataliwa mara moja, utakosa wanawake wengi sana wanaokupenda kwa dhati.


Baadhi ya wanawake hukataa unapowajia mara ya kwanza na kuwaambia hisia zako lakini moyoni mwao wanakupenda. Huwa wanakataa ili kukupima tu kama unaupendo wa kweli au unawajaribu. Yani wanawake wengine wanaweza kukubali baada ya kuwaelezea zaidi ya mara tatu.

Leave a comment