Kupoteza simu ni jambo ambalo linaweza kumtokea mtu yeyote na linaweza kuwa na athari mbaya katika maisha yetu. Simu zetu zimejaa taarifa muhimu, picha za kumbukumbu, na mawasiliano ya shughuri zetu nyingine muhimu. Wakati simu inapopotea au kuibiwa, inaweza kuleta hasara kubwa, si tu kwa kwenye akili bali pia kwa taarifa binafsi na usalama wa mwenyewe simu.
Kuna mamilioni ya simu hupotea kila mwaka Duniani Kwasababu mbalimbali na wengi huwa hawazipati simu zao. Simu inapopotea, mtu anaweza kuingia kwenye hatari za kupoteza taarifa binafsi kama vile akaunti za benki, chats muhumu, na Akaunti za mitandao ya kijamii. Bila simu, tunaweza kupoteza mawasiliano na marafiki, familia, na hata kazi tunazofanya. Hali hii inafanya tukio la kupoteza simu kuwa na athari ya kufika mpaka kujaribu maisha ya mtu.
Katika ukurasa huu, tutaangalia njia mbalimbali ambazo zinaweza kukusaidia mtu kupata simu iliyoibiwa au kupotea. Njia hizi ni rahisi kufuata na zinaweza kusaidia kupunguza hasara na kurejesha mawasiliano yako haraka iwezekanavyo.
Game zenye muonekano mzuri za Online Battle Royale BONYEZA HAPA>>>
Njia za kutafuta simu iliyopotea au kuibiwa
Kuipigia au kutuma ujumbe kwenye namba iliopo kwenye simu
Njia ya kwanza unayoweza itumia kupata simu yako iliopotea na kuitumia ujumbe au kuipigia namba ya Laini (Sim card) iliopo kwenye simu. Kupiga simu kutafanya uongee na mtu alie na simu yako kama bado haijazimwa. Kama itakua haipatikani, tuma ujumbe au sms kwenye namba hiyo ili laini ikirudi hewani, upokee taalifa ya kuwa sms imefika (Delivered report) na kujua simu yako ipo imewashwa.
Hii ni njia nzuri na rahisi kuitumia kuitafuta hata simu ya batani ilioibiwa au kupotea.
Kutumia Find My Device kujua simu ilipo
Google Find My Device ni huduma ya Google ya Bure kabisa ambayo inawezesha watu kutambua simu zao zilipo kwa kuzionesha katika Ramani. Huduma hii inampa mtu nafasi ya kuifunga simu iliopotea au kufuta vitu vilivyomo ili visionwe na mtu mwingine.
Kutumia njia hii kupata simu iliopotea utatakiwa kudownload app iitwayo “Google Find My Device” kwenye simu nyingine. Baada ya hapo, utaifungua app hiyo na kujaza Email iliopo kwenye simu ulioibiwa kisha utaletewa taalifa za simu yako na sehemu iliopo.
Kama hiyo simu iliopotea itakua imeunganishwa kwenye internet alafu imewashwa Location, utafanikiwa kuiona ilipo na kuifuatilia. Lakini kama hivyo vitu vitakua vimezimwa, hautafanikiwa kuona simu yako ilipo.
Kwa watu wa iPhone, Find My Device ya Google haiwezi wasaidia maana ni maalumu kwa simu za Android. Ukiwa na iPhone utahitaji kutumia huduma kutoka Apple inaitwa “Find My” au “iCloud Find My Devices“.

Kutumia IMEI kupata Simu ilioibiwa
Utapatikanaji wa Simu iliopotea au kuibiwa ni ngumu kufanywa na mtu binafsi kwa njia hii. Jambo hili linahitaji uhusishe polisi na utatakiwa kuwa na Sababu ya kufanya hivyo maana police au vyombo vya usalama hawatakusaidia kama umeipoteza wewe mwenyewe kwa uzembe wako au umesahau ulipoweka. Ni vema kuwa na Sababu ya msingi na inayopelekeaa kuwahusisha polisi au vyombo vya usalama.
Mwisho ningependa kusisitiza swala la kuweka vitu vyako ikiwemo simu, katika hali ya usalama. Epuka kuweka simu yako mbali na mifuko yako au mikononi mwako unapokua mbali na nyumbani.