Kuwasiliana na mpenzi aliembali kunaweza kuwa na changamoto, lakini ni jambo muhimu linaloweka mahusiano katika hali nzuri. Umbali unaweza kuwa ni Sababu ya mahusiano mengi ya mapenzi kuvunjika. Kuna watu hujikuta wamepoteana kabisa na wapenzi wao baada ya kuwa mbali kwa muda mrefu.
Lakini sio kila mahusiano yanaweza vunjwa na umbali, Kuna watu hudumu pamoja hata wakiwa mbali. Na jambo hili linawezekana mkipendana.
Kuna mambo madogo ambayo yanaweza kusaidia kuimarisha uhusiano wenu na kuhisi kama mnaishi pamoja. Katika kurasa hii, tutazungumzia mambo hayo madogo ambayo yanaweza kufanya tofauti kubwa katika mawasiliano na mpenzi aliembali.
Mambo haya yanaweza kusaidia kupunguza kuuhisi umbali kati yenu na kuhakikisha kwamba uhusiano wenu unakua vizuri. Lengo la kufanya hivi ni kusaidia watu waliopo kwenye hali hii kujisikia wapo karibu pamoja na hata kuyalinda mahusiano.
Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze kila mara BONYEZA HAPA>>>
Mambo madogo ya kuzingatia katika kuwasiliana na mpenzi aliembali
Kuuliza alipo mnapowasiliana na anacho kifanya
Unaweza sikia mara nyingi kuwa watu hawapendi kuulizwa “upo wapi sasaivi?” lakini usiache kumuumiza mpenzi wako swali hilo. Ni muhimu kufahamu mpenzi wako yupo sehemu gani hatakama mahali alipo ni sehemu usiozo zijua vizuri. Mbali na mahali alipo, unaweza muuliza na kitu anacho kifanya pia.
Ukiwa na tabia hii unapowasiliana na mpenzi aliembali itakusaidia kuelewa maisha anayoishi na pia mizunguko yake. Kupata picha ya mizunguko au maisha yake kunaweza fanya muwe kama muko pamoja mnapo wasiliana. Tabia hii ni kama inaunganisha ulimwengu wenu hivi. Inaweza kufika mahali mnapiga stori kuhusu mambo anayoyaona, sehemu alipo, sehemu anayoelekea na hata changamoto anazokutananazo alafu mnaelewana.
Hali ya kutafutana
Umbali unaweza fanya mahusiano kufifia lakini mawasiliano yanaweza kudumisha mahusiano. Watu wengi hutumia simu kama njia ya mawasiliano na wapendwa wao waliombali.
Endapo kutafutana kwenye simu kutafifia na hakuna njia nyingine ya mawasiliano, basi mahusiano yanaweza kuwa hatarini sana.
Ni vema kuzingatia hali ya kutafutana na kuhakikisha ipo vizuri kati yenu maana kufifia ni dalili mbaya. Hakikisha unamtafuta mpenzi wako na pia usisahau kufanya mambo yanayofanya asikusahau.
Kutumia maneno mazuri ya upendo
Kuwasiliana na mpenzi wako na kuzungumza kama mafiki sio jambo baya ila usinisahau kuwa unahitajika kuongea nae kama mpenzi wako. Unahitajika kutoa maneno mazuri yatakayo ugusa moyo wake. Kumkumbusha kuwa unampenda, mwambie maneno yatakayo msisimua mpaka akuite “romantic”. Usipofanya hivyo kuna mtu wa karibu yake anaweza fanya hivyo na kuuteka kirahisi moyo wa mpenzi wako aliembali. Akisifiwa au kuchokozwa kidogo vile ambayo wewe haumchokozi, anaweza kukuweka pembeni utulie na mazungumzo yako ya kirafiki.
Sms za kumsifia mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>
Kufanya vitu zaidi ya mawasiliano
Mawasiliano yanaweza kuwashikilia mnapo kuwa mbali na mpenzi wako lakini ni muhimu kufanya vitu zaidi ya mawasiliano pia. Mnaweza fanya vitu kama kutumiana zawadi, pesa na kufanya mambo mengine ambayo mtu unaweza kusema “Mpenzi wangu aliembali amenifanyia” mbali na maneno maneno.
Natumaini hayo yanaweza kuwa msaada kwako kama upo katika hali ya umbali na mpenzi wako wa kiume au wa kike. Ukiwa mwanamke au mwanaume mambo haya ni muhimu kuyajua maana kuwa mbali na mtu unaempenda kunaweza tokea kwasababu nyingine zisizozuilika.