Maswali ya mwanamke yanayohitaji umakini kujibu (Fikilia kwanza)

Mwanamke anaweza kuwa na maswali mengi ukiwa nae kwenye mahusiano. Maswali haya yanaweza kutokea kutokana na hali mbalimbali zinazomkabili, ikiwa ni pamoja na masuala ya afya, mahusiano, kazi, na hata utani tu. Sio kila swali analouliza mwanamke ulienae kwenye mahusiano lina umuhimu au linahitaji umakini. Laini baadhi ya maswali hayo yanahitaji kufikiriwa kwa kina ili kutoa majibu yanayofaa.

Ukiwa kama mwanaume ni muhimu kuwa na uelewa wa kutambua maswali muhimu toka kwa mwanamke. Mwanamke ulienae kwenye mahusiano akikuuliza maswali usijibu vyovyote unavyojisikia tu, jaribu kufikilia kabla haujajibu. Baadhi ya maswali yanaweza kuwa kama mepesi lakini ndio yakawa ni mazito kuliko mahusiano yenyewe.

Mwanamke anaweza kukuwinda mwezi mzima ili akuulize swali dogo sana kwako lakini jibu lako linaweza kuwa na maana kubwa kwake. Usipo mridhisha na majibu yako anaweza kukujia tena na swali hilo hilo au akaliuliza kwa mtindo mwingine.

Katika makala hii, tumechambua maswali machache ambayo mwanamke anaweza kuwa nayo, maswali ambayo yanahitaji umakini katika kuyajibu. Kujua haya inaweza kukusaidia mwanaume kijana katika mahusiano ya mapenzi na mwanamke.

Jinsi ya kujua mpenzi ulienae anakupotezea muda BONYEZA HAPA>>>

Maswali ya mwanamke yanayohitaji umakini kuyajibu

Unamalengo gani na mimi?



Mara nyingi wanawake ukiwanao kwenye mahusiano wanaweza uliza Swahili na huwa zito sana japo ni kama jepesi. Mwanamke mpaka kafikia hatua ya kukuuliza swali hili tambua amejiuliza vitu vingi sana kichwani kuhusu mahusiano yenu na anataka uyajibu wewe kwa hilo jibu utakalo litoa. Ukijibu jibu ambalo litamuonesha hauna mpango mzuri nae basi mahusiano kwanzia hapo yanaweza anza kukata muda wowote.


Huwa mara nyingi wanauliza swali hilo ili kujua mahusiano mulioyaanzisha ni yakudumu au laa. Kama ataona umejibu kama hauna mpango nae basi anaweza anzisha mahusiano yoyote mapya muda huo. Unaweza kuta tu hata ameolewa ghafla na hajakwambia.

Unafanya kazi gani?



Wanaume wengi huwa wanajibu swali hili kirahisi lakini ni swali ambalo ukikosea kujibu mahusiano yako yanaweza kuwa magumu. Mwanamke ambae hajui kazi yako akikuuliza kuhusu kazi unayoifanya, usikurupuke kutaja kazi nzuri sana ili tu akupende. Ni bora utaje ya kawaida au usitaje kabisa.


Unapomwambia mwanamke kazi yako kuna jinsi kichwani anafikilia atakavyoishi na wewe na maisha yatakuaje. Ukiwa mtu mwenye kipato kidogo na anakupenda basi kunajinsi anaweza kuwa anajibana kimatumizi na kukuomba pesa ndogo kwenye shida.


Ukimwambia unafanya kazi nzuri na ina pesa, usishangae akianza kukuomba viasi vikubwa vya pesa na kukuletea matatizo yanayohitaji pesa nyingi. Sio wanawake wapo hivi ila wengi baada ya kujua kazi huwa hivyo. Kiufupi huwa wanapenda kuwa wanawake wa kiwango chako na ukidanganya kiwango, kunajinsi uweza shindwa kufurahia mahusiano maana atakua amejiweka kwenye kiwango kisicho chako.

Unanipenda kweli?



Hata ukiamshwa usingizi na mpenzi wako unaempenda, hakikisha unajibu vizuri hili swali. Mara nyingi mwanamke akikuuliza “Unanipenda kweli?” Anaweza kuwa anataka kuondoa wasiwasi moyoni mwake juu ya upendo wako kwake.

Inaweza kuwa sio kila anapokuuliza swali hili anawasiwasi ila kumjibu huwa kunaufanya moyo wake ujimwage zaidi kwako.
Kuna muda swali hili pia huwa na jambo kubwa nyuma yake. Lakini uzuri ni kwamba sura yake inaweza kukuambia kama ni jambo baya au zuri.

Umenipendea nini?



Mwanamke kukwambia “Umenipendea nini?” ni jambo la kawaida sana na mwanaume wengi husema “Nakupenda jinsi ulivyo tu”. Mwanaume ni bora ujibu hivyo kuliko kujibu vingine ukajichanganya.


Kuna wanawake huwa wanatafuta mwanaume anaewapenda kweli jinsi walivyo na sio kuwatamani. Ukikutana na mwanamke ambae yupo hivi alafu akajibu mambo kama “Shepu” au “Macho” na vingine bila kumwambia kwanza umempenda jinsi alivyo, anaweza kuweka kwenye kundi la waliomtamani.
Ni vema ukamwambia kwanza umempenda jinsi alivyo alafu akataja na vitu vingine vinavyokuvutia zaidi au unavyo vitamani.



Maswali haya machache ni ya msingi na mara nyingi yanakua na machango mkubwa kwenye kuimarisha mahusiano. Kila swali lina maana yake na uzito wake, na unatakiwa kuyajibu kwa uangalifu. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Leave a comment