Ni muhimu kuzingatia na kuheshimu hisia na mahitaji ya mwenzi wako. Hili lina umuhimu mkubwa zaidi kwa wanawake, ambao mara nyingi wanahitaji uangalifu maalum ili kuhisi kuthaminiwa na kuungwa mkono ndani ya mahusiano na hata maisha kiujumla. Hapa The bestgalaxy ukurasa huu unaenda kukujuza mambo ambayo si vema ukayafanya kwa mwanamke unapokua nae kwenye mahusiano. Makala hii inaweza onekana imelenga mwanaume lakini kila mtu anaweza isoma. Mbali na hayo kuna makala nyingine tutakuja lenga wanawake pia na itaweza somwa na yoyote.
Katika Mahusiano mnaweza kutana na watu wenye tabia tofauti, mkaelewana na kuwa pamoja. Kuwa pamoja kama wapenzi kunaweza kuwa na mambo mengi sana mnafanya au kufanyiana. Mambo mengine yanaweza onekana mazuri na mengine yakaonekana wazi kuwa mabaya. Mengine yanaweza kuonekana mazuri au ya kawaida lakini ni mabaya baada ya muda.
Jinsi ya kumfurahisha mwanamke katika Mahusiano BONYEZA HAPA>>>
Mambo mwanaume kumfanyia mwanamke si vizuri
Usitoe siri au mambo mabaya ya mwanamke wako kwa wengine
Unaweza ukawa na mpenzi mwanamke mwenye mambo ambayo si vema kuyaonglelea kwa watu. Yanaweza kuwa ni mambo yanayofanya mtu amshushe thamani na kumchulikia vibaya.
Ikiwa unatabia ya kuongea mambo hayo kwa watu na bado upo nae kwenye mahusiano hata wewe unaemuongelea unakua unajichafua pia. Itakua ni vizuri kama utakua unatabia ya kutomuongelea vizuri mwanamke wako maana thamani yake ikiwa kubwa kwa watu na wewe unaonekana wathamani pia. Ni bora usimuongelee kabisa kuliko toa Siri au kumuongelea vibaya mtu ulienae kwenye mahusiano.
Usimshawishi kufanya mambo hatari kupinga ujauzito
Kama unampenzi na hamjafikia hatua ya kukubaliana kuzaa, basi hakikisha ukiwa kama mwanaume unakua mungalifu pia kwenye kuzuia ujauzito. Usiwe ni mtu ambae unaenda mara kwa kama hauoni au kuelewa mwanamke anatumia njia zipi alafu anakua makini kusisitiza mwanamke atumie njia hatari kuzuia matokeo ya uzembe.
Njia hatari zikizidi zinaweza msababishia mwanamke matatizo ya kizazi. Sasa unaweza muelewa kirahisi pindi atakapo patwa na matatizo hayo na kushindwa kupata ujauzito?
Ukiona mwanamke wako haelewi au anatumia sana njia za hatari bila kukushirikisha, hakikisha unamsaidia na kumuelimisha. Sio Kila mwanamke anaufahamu mzuri juu ya mambo ya uzazi. Fanya hivyo ili muuzuie ujauzito kwa njia salama na awe vizuri mpaka mtakapo amua kupata mtoto.
Jinsi ya kum-surprise au kumshangza mpenzi wako bila kutumia Pesa BONYEZA HAPA>>>
Usimpuuze bila kumsifia au kumpa maneno mazuri baada ya tendo
Baada tu ya tendo hasa la mara ya kwanza kwa mwanamke anaweza kuwa na mawazo mengi ya kutaka kujua kama yupo vizuri kwako au laa. Ukiendelea na mambo yako na kuondoa ukaribu baada ya tendo Hilo unaweza kumfanya mwanamke ahisi vibaya juu yake mwenyewe.
Kama ni mpenzi wako, hakikisha haumuachi kwenye Mawazo hayo kila mara. Jitahidi kukumbuka kumtafuta na kumpa maneno mzuri juu ya alicho kufanya na wewe. Hii pia inaweza kumfanya ajiamini au kuwa huru anapokutana na wewe tena kwenye tendo.
Epuka mahusiano ya muda marefu kama haunampango wa kumuoa
Kati ya mwanamke na mwanaume, mahusiano yakianza mara nyingi anaewaza mbali kuhusu mahusiano ni mwanamke. Anaweza waza kuhusu familia na hata watoto kipindi mahusiano hayajafikia hata kuishi pamoja. Hili sio jambo baya maana ni moja ya ndoto zao.
Unapokua na mwanamke kwenye mahusiano ya muda mrefu anaweza kuwa anawekeza sana akili yake kwako na kufanya amini utakua nae milele. Sasa kama hauna mpango wa kumuoa au kuwa nae maishani basi ni wazi mahusiano ya muda marefu ni maandalizi ya kumuumiza tu. Ikiwa hautaki kumuumiza mwanamke usie na mpango nae, mahusiano ya muda mrefu ni yakuyaepuka sana ili usimuuze. Usipofanya hivyo unaweza uumiza na kumpotezea muda wa kumtafuta atakae mpenda milele au kumuoa.
Mambo tuliozungumzia hapo juu yanaweza kuwa marahisi kusahau au kupuuza lakini ni mambo muhimu. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy na useache kuwa nasi.