Vichekesho vya kiswahili vunja mbavu




Karibu kwenye makala hii yenye vichekesho vya kusoma vinavyofurahisha! Katika ulimwengu wa hadithi za kuchekesha, tunakuletea mkusanyiko wa visa vya kufurahisha na kukuvunja mbavu. Kupitia makala hii, utaweza kufurahia na kucheka kwa kujitupa katika hadithi fupi zilizojaa kujifunza na kuchekesha pia.

Hadithi hizi za kuchekesha zimeandikwa na watu kwa ustadi na kubuniwa kwa kina ili kukuvutia wewe msomaji lakini hapa the bestgalaxy, zimekusanyawa tu. Hadithi inaweza kuja na mchanganyiko wa utani, kujikosoa, na vituko, kikubwa usiwe serious sana, lengo kubwa ni kucheka kufurahi hivyo jiachie.


Kucheka ni moja ya mambo muhimu katika maisha yetu ya kila siku. Kwanza kabisa, kucheka husaidia mtu kupunguza msongo wa mawazo na hali ya wasiwasi. Unapocheka, mwili wako huzalisha homoni za furaha kama vile endorphins, ambazo husaidia kupunguza mkazo na kuongeza hisia za nzuri.

Vichekesho vya kiswahili vunja mbavu

MUOKOTA MAKOPO:

Tamaa mbaya! Muokota makopo katika uokotaji wake wa makopo akaona chupa ambayo ndani kuna kikaratasi, alipoifungua chupa likatoka jitu la ajabu lisilo onekana na watu wengine. Lilikua likitetemeka na lilimwambia “kijana asante sana kwa kuniokoa omba vitu viwili sasa hivi”. Kijana kwa hofu akaomba pesa za kumiliki magari na majumba ya kifahari. Ghafla fuko liliojaa hela na pete ya dhahabu ya bahati vikadondoka mbele yake. Akaambiwa aseme ombi la pili, akasema “Nibadilishe niwe kivutio ili nipendwe sana nakina dada wazuri” Hapohapo jamaa akageuzwa akawa chipsi yai.!!

MTOTO MDOGO KATULIA NA BABA:

MTOTO: Hivi Baba ivi wewe umezaliwa wapi?
BABA: Nimezaliwa Mbeya
MTOTO: Mama nae kazaliwa Mbeya?
BABA: Hapana, amezaliwa Tanga
MTOTO: Na Mimi jee?
BABA: Dar
MTOTO: Mh Sasa tulikutanaje????
Baba akaangua kicheko

JAMAA BAADA YA KUCHELEWA KAZINI:

Boss: kwa nini umechelewa kazini

Juma: kuna mtu njiani alidondosha 5000 boss

Boss: anha kwahiyo ulikua unamsaidia kuitafuta

Juma: Hapana, bahati nzuri niliikanyaga nikawa nasuri aondoke.

MAWAZO YA VIKOBA:

(Mdada baada ya kufika kwa mpenzi wake akiwa na Mawazo mengi ya vikoba)

Mdada: Baby, naomba shilingi elufu kumi na tano nilipie taxi niliokua nayo.

(Mkaka kaingiza mkono mfukoni kutoa pesa lakini ghafla alipomuangalia mpenzi wake vizuri akashtuka!)

Mkaka: Unasema umekuja na Taxi? Mbona umejisahau umekuja na helmet ya Bodaboda?

Katika ukurasa huu, tuliokuandalia ni hayo tu lakini Kuna vichekesho vingi ndani ya The bestgalaxy ambayo unaweza furahia kuvisoma. Endelea kuwa karibu na sisi kwenye mambo mbalimbali tunayojihusisha nayo.

Stori za vichekesho vya kuvunja mbavu BONYEZA HAPA>>>

Leave a comment