Jinsi ya kutengeneza Pesa kwa AI za kuunda Picha

Al za kutengeneza au kuunda picha zipo nyingi sana sasa na hata watumiaji wake ulimwenguni wapo wengi pia. Kuna AI ambazo huunda picha kutokana na maelezo ya maneno inayopata na nyingine huwa zinaweza kuunda picha mpya kutokana na picha iliopewa. Yote hii ni kumuwezesha Kila mtu kuwa na uwezo wa kutengeneza picha anayoifikilia au kuihitaji. Kiufupi wanasema AI hizi zinakusaidia kugeuza wazo au unachofikilia kuwa katika picha.
Watu huzitumia AI za kutengeneza au kuunda picha katika mambo mbalimbali ikiwemo kutengeneza pesa.

Kunawatu mpaka kufikia sasa AI kwa ujumla imewasaidia kutoka sehemu moja kwenda nyingine kibiashara au chumi na mambo mengine, ikiwemo hizi za kuunda picha. Kwaiyo kutengeneza pesa kupitia AI za kuunda picha ni jambo liliofanywa na watu na linawezekana pia. Hapa Kwenye ukurasa huu the bestgalaxy tunakufungua juu ya namna gani mtu unaweza ingiza pesa au kutengeneza pesa kupitia hizi AI za kuunda picha.

AI za kutengeneza picha kwa kutumia maneno BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kutengeneza Pesa kwa AI za kuunda Picha.

Kuprint nguo ya picha za AI na kuuza

Unajua kwamba kuna nguo zina picha zinauzwa madukani na zinapendwa na watu kutokana picha hizo lakini ukifuatilia utagundua picha hizo zimeundwa na AI? Unaweza fanya hivi pia kama unataka kutengeneza pesa kwa AI za picha. Unaweza tafuta nguo uka print picha zuri ya kuvutia iliotengezezwa na AI, hasa T-shirt. Alafu baada ya hapo ukaziuza kwa bei inayoendana na muonekano wake. Kama picha itakua nzuri na kuvutia, unaweza uza sana nguo za mtindo huu. Lakini hii ni nzuri kuijaribu kama una Duka la nguo au unajihusisha na maswala ya nguo ili usipate shida mambo yakiyumba kwenye mauzo.

Mfano wa nguo ni hii T-shirt nyeusi yenye picha iliotengenezwa na AI

Kukuza page ya picha za AI na kuimonetize

Kwenye mitandao ya kijamii inayojihusisha na picha, kama vile Facebook au Instagram, unaweza tengeneza pesa kwa AI. Utakachotakiwa kufanya ni kuhakikisha unaposti picha nzuri kwenye ukurasa(page) wa Facebook au Instagram bila kuchoka mpaka utakapo pata watu wengi wanaoungana na wewe kwenye kurasa yako. Huo ukurasa inabidi ujihusishe na kitu jambo ambalo unalielewa sana kwenye maisha yako na unaweza wasaidia wangine kwenye jambo hilo. Na picha utakazokua unapost utakua unatengeneza kwa Al alafu zinatakiwa kuwa zinahusu mada moja ulioichagua. Kama unataka kujihusisha na magari, basi picha unazotengeneza inabidi ziwe za kuhusu magari. Unapoziposti unaweza ziwekea maelezo ambayo yatamvutia mtu kusoma au kujifunza.
Kama utafanikiwa kuwa na watu wengi unaweza anza toa huduma kwa watu au kuuza vitu ili upate pesa. Unaweza kuwa unalipwa pia kama na watu wengine kwa kuonesha matangazo.

Kutengeneza video kwa picha na kwenye platform zinazolipa

Kama ni mtu wa kutengeneza video, AI za kutengeneza picha zimekuja kukukomboa kwa kiasi kikubwa sana. Kuna aina za video huwa haziitaji vitu vingi katika kuzitengeneza, zinahitaji sauti na picha. Sasa AI kama inaweza kukupa picha kirahisi basi kutengeneza video za namna hii kwako inakua nirahisi kuliko kutumia picha zenye copyright. Na jambo hilo likiwa rahisi kwako inamaana unaweza tengeneza video za mtindo huo na kupelekea kwenye platform kama YouTube, Facebook au YouTube alafu ukapambana ukalipwa. Hata ukishindwa kulipwa na hizo platform unaweza tengeneza mfumo wako wa biashara utakao kulipa.

Kutengeneza watu matangazo ya biashara

Kama ni Graphics designer unaeweza tengeneza matangazo ya biashara, AI za picha zinaweza kukufanya uingize pesa pia. Kupitia AI unaweza tengeneza picha ya mtu au vitu vingine unavyohitaji kwenye kuunda tangazo la biashara. Kuna baadhi ya makampuni kwasasa yanapeperusha matangazo yalioundwa Graphics designer kwa msaada ya AI. Yani unawezamuona mtu kwenye tangazo lakini mtu huyo ametengenezwa na AI.
Hii ni njia hai kabisa na inatumika mpaka sasa na Graphics designers wengine kuweka kazi zao kwenye hali ya juu na kutengeneza pesa kirahisi. Kikubwa ni usitumie AI kukupa inachotaka, Itumie AI kupata unachotaka ili uendelee kuwa creative.

Mwisho ningependa kukukumbusha kuendelea kuwa karibu na mambo ya AI ili uelewe jinsi ya kuzitumia. Ni muhimu sana kwa mtu kuelewa AI katika miaka hii ili usije achwa nyuma kibiashara na kwenye mambo mengine.

Leave a comment