Jinsi ya kuongeza ubora wa picha zako za zamani kwenye simu

Unaweza piga picha yenye ubora kwenye simu yenye kamera nzuri lakini baada ya muda au kipindi flani ukawa na picha hiyo uliopiga ikiwa inaonekana haina ubora. Picha hiyo ya zamani unawezaona haina ubora baada ya kupitia kwenye mitandao ya kijamii na michakato mingine inayopunguza ubora wa picha. Mbali na hayo, baada ya kupata simu yenye kamera inayotoa picha zenye ubora zaidi, unaweza anza kuona picha ya zamani haina ubora.

Nikawaida watu kuwa na picha zao wanazoziona hazina ubora na kama ni mmoja watu hawa, hapa The bestgalaxy tunakupa mwanga kuhusu kuziongeza ubora. Unapokua na picha zisizo na ubora, kumbuka kuna huduma zinazokuwezesha kuongeza ubora wa picha. Huduma hizi ni software ambazo nyingi huiongezea picha ubora bila kukuhitaji ufanye vitu vingi. Zimewezeshwa na AI hivyo ni rahisi kutumia kiasi ambacho mtu yoyote anaweza tumia kuongeza ubora wa picha zake.

AI ni nini na inaleta matokeo gani katika Ulimwengu? BONYEZA HAPA>>>>

Jinsi ya kuongeza ubora wa picha zako za zamani kwenye simu za Android

Kwenye simu za Andoid kupata huduma ya kuongeza ubora wa picha, unaweza tumia app iitwayo UpFoto. App hii inatumia internet ila inaweza pandisha ubora wa picha yako bure na rahisi sana kuitumia. Ukihitaji kujaribu kwenye picha zako zilizopoteza ubora, fuata maelezo yafuatayo;

 

  • Nenda katika Playstore na uipakue app iitwayo UpFoto kwenye simu yako.
  • Fungua, chagua Lugha ya “English” alafu bonyeza “Start” kwenye ukurasa utaopelekwa.
  • Baada ya hapo bonyeza kitufe cha “Try now” kwenye sehemu ilioandikwa “Enhance” kisha uchague picha unayotaka kuiboresha.
  • Baada ya kuchagua, Bonyeza kitufe kilicho andikwa “Enhance” ili kuanzisha mchakato wa kuboresha hiyo picha.  
  • App ikimaliza mchakato, utaletewa picha ilioboreshwa alafu utatakiwa kubonyeza kitufe kilichoandikwa “Save” ili kuiweka picha hiyo kwenye simu yako.

Kwa kufanya hayo utakua umefanikiwa. Lakini unapaswa kujua kwamba app ya UpFoto inamatangazo ambayo utakua unakutana nayo katika kufuata hatua hizo. Mbali na matangazo, app hii itakuomba access chache kwenye simu yako na utakua unabonyeza “Allow” kuiruhusu.

Kama ubora utakua haujakulidhisha unaweza chukua picha iliotoka kwenye app hiyo, alafu ukairudisha kwenye app kuiongeza ubora kwa mara ya pili.

Leave a comment