Jinsi ya kujiondoa kwenye post mbaya ulizoshirikishwa Facebook

Facebook inaruhusu kushirikisha mtu kwenye picha au post yako na huwa tunaita ku “Tag”. Mtu unaemshirikisha kwenye post yako anatakiwa kuwa ni rafiki yako wa Facebook. Kumshirikisha mtu ambae hamna urafiki kwenye Facebook haiwezekani kwa kumtag ila unaweza tumia kipengele cha kutaja (mention) kama njia ya kumshirikisha mtu.


Mtu unapo shirikishwa kwenye post kwa kipengele cha “Tag” na rafiki yako mmoja, marafiki zako wengine wanaweza pata taharifa kuwa umeshirikishwa kwenye post hiyo. Na endapo picha ulioshirikishwa itakua ni picha mbaya au usio taka kushirikiswa, Bado unauwezo wa kujiondoa.

Jinsi ya kujua kama akaunti yako ya Facebook ni Salama BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kujiondoa kwenye post mbaya ulizoshirikishwa Facebook

Hapa chini tunaenda kukuelekeza hatua kwa hatua jinsi ya kujiondoa kwenye post waliokutag katika Facebook lakini hautaki kuhusishwa. Jambo zuri ni kwamba ukijiondoa, aliekutag hawezi pokea taharifa kuwa umejiondoa.
Ili mtu kugundua kuwa umejiondoa kwenye post aliokushirikisha itambidi azingatie vitu viwili. Cha kwanza ni idadi ya watu aliowashirikisha na Cha pili ni kuzingatia uwepo wa jina lako kwenye orodha ya watu aliowashirikisha. Watu wengi hawazingati jambo hili wanapo post picha na kushirikisha wengine katika Facebook japo.
Unaweza fuata hatua hii kuondoa Tag

  • Ingia katika Facebook na uende Katika post waliokutag
  • Bonyeza vidoti vitatu vilivyo upande wa pembeni katika post hiyo.
  • Chagua “Remove Tag” kwenye orodha ya chaguzi utazoziona.
  • Bonyeza”CONFIRM” ili kuthibitisha maamuzi yako ya kujiondoa kwenye post hiyo.

Ukisha fanya hivyo tu, post itakua uhusiano na wewe tena. Utakua umefanikiwa kujiondoa kwenye post hiyo na kama ilikua inaonekana kwenye orodha ya post zako, itaondolewa. Lakini kama ikitokea watu wengine au post mpya unaweza shirikishwa tena kama kawaida.

Leave a comment