Jinsi ya kujua kama simu inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine(anaona bila kuigusa)

Katika matumizi yako ya simu za Smartphone unatakiwa kuelewa kwamba vifaa hivi vinaweza kudukuliwa na mtu mwingine na kufanya mdukuzi au huyo mtu apate uwezo wa kuona vitu vilivyomo au vitu unavyofanya kwenye simu yako bila yeye kuigusa simu yako. Mbali na kuona vitu unavyofanya au ulivyohifadhi, Mtu aliedukua simu yako pia anaweza kuwa na uwezo wa kuitumia simu yako bila kuigusa… Mfano wa vitu anavyoweza kuvifanya ni kuitumia simu yako kutuma sms kwa mtu mwengine, kuitumia camera yako kuangalia unachokifanya, kuvujisha vitu vyako au kukuzuia kufanya baadhi ya vitu kwenye simu yako.

Lakini ukiwa kama mtumiaji wa smartphone wa miaka hii, hutakiwi kuwa na hofu sana juu ya hili kwani kunaviashilia vya kuangalia kwenye simu yako ili kujua upo salama au vipi. Hapa The beestgalaxy tutakupa mwanga juu ya jinsi ya kuangalia simu yako ya Android kama imedukuliwa na inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Jinsi ya kuangalia kama simu yako inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine

katika matumizi ya simu watu huwa wanapenda kuingiza apps nyingine mbali mbali ukiachana na zile ambazo huwa wanazikuta tayari zipo kwenye simu. Kitu unachotakiwa kujua hapa ni kwamba kuna Program au apps ambazo unaweza kuingiza kwa bahati mbaya au ukaingiziwa kwenye simu yako na zikiwa kwenye simu yako zinakua zinatumika na mtu mwingine huona au kufanya vitu kwenye simu yako bila kuigusa.

Endapo katika simu yako kutaingizwa apps hizi kwa makusudi au bahati mbaya, simu yako itakua sio salama tena maana vitu. Lakini kitu kizuri ni kwamba kwenye sikuizi kwenye simu za Android kuna program inaitwa “Google play protect”. Program hii inamilikiwa na google na kazi yake kubwa kwenye simu ni kukulinda dhizi ya apps hatari unazoziingiza kwenye simu yako. Kama kuna app yoyote inayoweza kuwa hatari umeiingiza, Google play protect huwa inatoa taharifa na kukushari cha kuifanya. Unaweza kuitumia Google play protect kuangalia kama angalia kama simu yako ni salama au si salama. Unachotakiwa kufanya ni kufuata hatua hizi chini.

  • Chukua simu yako na uingie katika app ya Play store
  • Baada ya hapo, gusa kiduara cha profile yako na uchague “Play protect
  • Bonyeza kitufe kilichoandikwa “Scan” na baada ya hapo Google play protect itaanza kuangalia kama kuna app zozote hatari kwenye simu yako alafu itakupa majibu.
  • Kama kutapatikana app yoyote hatari utaonyenshwa app hiyo alafu utashauriwa kuiondoa kwenye simu yako kwa kugusa kitufe cha “Uninstall“.

Google play protect ni njia nzuri na rahisi ya kuangalia kama simu iko salama ukiwa kama mtumiaji wa kawaida lakini huwa haikuhakikishii usalama kwa 100%.

Google play protect ikiwa “Active” kwenye simu yako huwa inatafuta na kulinda hii ya app hatari. Na endapo itakuta app harari imeingizwa au unataka kuiingiza kwenye simu yako, itakupa taharifa.

Mbali nna kutumia Google play protect kuangalia kama simu yako iko salama unaweza pia kujua kuwa simu kwa kuangangalia kama kwenye simu yako kuna vitu vifuatavyo.

Angalia orodha ya app zinazotumia sana internet na kama utakuta app ambayo haieleweki na hauitumi lakini ipo juu kwenye matumizi ya bando, inawezakua ni app hatari. Kama kamera ya simu yako ukiifungua inakuandikia “Camera is being used by another application” au “You cannot use more than one application that uses camera” au “Camera may be in use by another application” hiyo inaweza kuwa ni ishara ya kwamba simu yako sio salama. Mbali na hayo, kukuta vitu ambanyo haujavifanya lakini vimefanyika kunaweza kuwa kiashiria cha hatari pia.

Leave a comment